Sina shaka umeshasikia kuwa Rais Kikwete hivi karibuni alipokuwa Marekani alikutana na hit maker wa ‘Number 1’ Diamond Platnumz, na akamuunganisha na mmoja wa wadau muhimu katika muziki duniani Kevin Liles, ambaye ni meneja wa Trey Songz ili amsaidie.
Rais Kikwete alimpomkutanisha Diamond na Kevin Liles
Hivi sasa Mr President ametoa shavu lingine kwa wasanii wote wa muziki na filamu kwa kuwaletea wadau muhimu katika tasnia ya sanaa duniani, akiwemo muimbaji maarufu wa Marekani Usher pamoja na mtangazaji wa E! Entertainment Television, Terrence Jekins aka Terrence J.
“Siku ya pili akaja kiongozi mwingine Chaka Zulu, Shakazulu huyu ndiye meneja wa Ludacris[…] amekuja Chaka zulu tumezungumza naye, na wote hawa hatimaye tumekubaliana kwamba watakuja[….] watakuja tarehe 11 July mpaka tarehe 23 July”. Alisema Rais Kikwete.
Aliendelea,
“Anakuja Terrence J, Terrence J huyu ndiye muasisi wa Black Entertainment Television, lakini sasa Terrence J ndiye anaendesha wale wanaoangalia kwenye televisheni Channel E! lakini Terrence J anakuja na mwanamuziki maarufu wa Marekani Usher, na bado hatujamaliza na Trey Songz anaweza kuja”. Alisema Rais Kikwete.
No comments: