Bill Clinton aliyekuwa Rais wa Marekani katika kipindi ambacho Mandela pia alikuwa madarakani, pamoja na mkewe Hillary pia watakwenda Afrika Kusini.
Viongozi wengine wa kimataifa wanaotarajiwa kwenda Afrika Kusini ni waziri mkuu wa Uingereza David Cameron, ambaye ataambatana na Prince Charles.
Kwa mujibu wa ratiba ya kuelekea siku ya mazishi, tukio kubwa la kwanza litakuwa ni December 10, ambapo ‘memorial service’ itafanyika katika uwanja wa mpira Johannesburg, wenye uwezo wa kubeba watu 94,000 uliotumika katika fainali za kombe la dunia 2010, ambapo maelfu ya watu watapata nafasi ya kumuaga Mandela.
Utaratibu wa maandalizi ya mazishi ya mzee Mandela uliandaliwa zaidi ya mwaka mmoja uliopita, kipindi ambacho afya yake ilipoanza kuwa mbaya, hii ni kwa mujibu wa The Guardian ambayo inasemekana kuwa na nakala yake.
Serikali ya Afrika Kusini imesema mazishi ya Mandela yatafanyika Jumapili ya wiki ijayo (December 15), katika kijiji alichokulia cha Qunu.
SOURCE: MAIL ONLINE
No comments: