Home
»
celebrity News
»
News
»
Pator Myamba
» EXCLUSIVE: PASTOR MYAMBA AKIZUNGUMZIA JUU UCHAWI ULIOTUMIKA KWENYE MOVIE YAKE YA GOD'S KINGDOM
Mwigizaji mkongwe na anayefanya vizuri sana kwenye tasnia ya filamu Tanzania Emmanuel Myamba maarufu kama Pastor Myamba, alifanya mahojiano na Bongo61 Team juu ya filamu yake mpya ya God’s kingdom atakayoizindua rasmi taerehe za mwanzoni mwa mwezi wa Mei. Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano hayoa yaliyofanyika ndani ya ofisi ya Chuo chake cha maigizo na filamu cha T.F.T.C Kilichopo ubungo Dar es Salaam.
Bongo61 Team: Tungependa kujua ni nini hasa kipo ndani ya filamu hii yako mpya ya God’s Kingdom.
Pastor Myamba: Aaah, kwa kifupi, God’s kingdom ni filamu inayoonesha uweza wa Mungu ndani ya maisha ya mwanadamu. Ni filamu inayyonesha ni jinsi gani Mungu ni mkuu na muweza wa yote tofauti na watu wengi wanayodhani kuwa mtu au kuna kitu kinaweza kumshinda Mungu.
Bongo61 Team: Kwanini umeamua kutengeneza filamu hii?
Pastor Myamba: Filamu hii ni mahususi kwa watu wanaoamini kuwa unaweza kumshinda Mungu kwa kutumia uchawi. Nataka watu waelewe kuwa Mungu ni zaidi ya kila kitu. Na nguvu za Mungu ni kubwa na ndio zenye mamlaka zaidi.
Bongo61 Team: Umeshirikiana na nani katika filamu hii?
Pastor Myamba: God’s kingdom imefanya kwa ushirikano na Patcho Mwamba na Jengua pamoja na baadhi ya wanafaunzi wa T.F.T.C.
Bongo61 Team: Huoni kuwa filamu hii inaweza kuleta mtafaurku kwa watu wanoamini mambo ya kishirikiana?
Pastor Myamba: Mmmh, unajua mimi kama msanii nina haki ya kuigiza kile nachoomini ni sahihi kwangu, filamu hii haijamlenga mtu yoyote, mimi kama kioo cha jamii natakiwa kuonesha kile ambacho naamini ni sahihi kwa jamii kukifuata.
Bongo61 Team: Kitu gani kingine ungependa kuwaambia mashabiki wako?
Pastor Myamba: Wakae tayari kushudia vipaji vipya toka katika chuo change cha sanaa na pia kwa wale wanaotaka kujifunza zaidi kuhusu sanaa na maigizo nasi wanakaribishwa sana kujiunga nasi ili wapate mafunzo bora ya kuwa waigizaji wazuri hapo baadae.
Bongo61 Team: Tunashukuru sana, na kila la kheri
Pastor Myamba: Asanteni sana.
Tunaomba Maoni yako Hapa :
Category: celebrity News News Pator Myamba
Related Posts
Fid Q amzunguzia mama wa mtoto wake Fidelie
Rapper Fid Q amesema ni mapema sana kuzungumzia masuala ya ndoa na mpenzi wake kutoka Jamhuri ya Cze...Read more »
26Sep2015Kajala Ammwagia Zari Minoti!
KIMENUKA tena! Katika kile kinachoonekana kama ni kejeli kwa shosti wake wa zamani, ambaye sasa pic...Read more »
25Sep2015Picha: Tiffah ni Photocopy ya Baba yake Diamond Platnumz
Tiffah, mtoto wa Diamond Platnumz aliyezaa na mpenzi wake wa Uganda, Zari the Bosslady ni kama photo...Read more »
25Sep2015Je Umeshawahi Kujiuliza Kama Kuna Ugomvi Wowote Kati ya Lulu Michael na Wema Sepetu...? Lulu Afunguka Haya
KAMA unafikiri kuna ugonvi kati ya waigizaji maarufu nchini, Elizabeth Michael, ‘Lulu’ na Wema Sepet...Read more »
25Sep2015Dk. Cheni Afunguka Kumuoa Lulu!
Tangu wakati ule msanii maarufu wa filamu, Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’ aamue kupambana kumsaidia Eliza...Read more »
25Sep2015Mama wa Diamond Aongelea Kuhusu Mjukuu wake Kuwa si Mtoto wa Diamond
Weekend iliyopita mtoto wa Diamond na Zari aitwaye Tiffah alitimiza siku 40 na sura yake kuonyeshwa ...Read more »
25Sep2015
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments: