Kiongozi mkuu wa kanisa Katoliki Papa Francis alikuwa akizungumza mbele ya umati mkubwa wa familia mbalimbali zilizohudhuria sherehe za siku ya familia. Baada ya mtoto huyo kupanda jukwaani alienda mbele ya papa na kumtazama na kuzunguka hapa na pale japo hakufanya fujo ya aina yoyote.
Makadinali walijaribu kutumia njia za kumshawishi kutoka kama kumpatia pipi, lakini mtoto huyo aligoma kuondoka. Papa alimgusa kichwani na kutabasam akamwacha na kuendelea na alichokuwa akikifanya.
Kuna wakati papa akiwa amesimama anazungumza mtoto huyo alimkumbatia miguu lakini papa alimwacha.

No comments: